IJUE VITA YA MCHANGA NA NGUVU ZA SAND MAFIAS



Mchanga: Ni moja kati ya maliasili zinazotumika kwa wingi Duniani. Ripoti za Umoja wa Mataifa zinaripoti kuwa, uchimbaji wa mchanga na kokoto unazidi Tani Bilioni 40 kwa mwaka, kwa sababu ya uhitaji mkubwa wa maliasili hiyo. Kuongezeka kwa matumizi ya maliasili ya mchanga kumesababisha ¾ ya fukwe za duniani tayari zimepunguwa kwa sababu ya ongezeko kubwa la matumizi ya mchanga (sand beach).

Mchanga ni maliasili inayotumika kwenye maisha yetu ya kila siku kwa matumizi mbalimbali kama vile ujenzi wa madaraja, nyumba, viwanja vya ndege na majengo marefu na kufanya kuwa moja ya maliasili muhimu sana kwenye shughuli nzima ya ujenzi wa mwanadamu. Mchanga pia unatumika kwenye utengenezaji wa microchips za computer (tarakilishi) na smart phones (sikanu). 

Katika sekta inayochukua asilimia kubwa ya mchanga ni sekta ya ujenzi. Karibia nusu ya watu Duniani hivi sasa wanaishi mijini. Inakadiriwa mpaka kufikia 2030 asilimia 60 ya watu duniani kote watakuwa wanaishi mijini. Ujenzi wa miji na kupanaku kwa miji mikubwa duniani inahitaji concrete na Asphalt zote zinatengenezwa kwa kutumia Mchanga.


“Ni sawa na hewa tunayoivuta, huwa atuifikiri sana, lakini hatuwezi kuishi bila ya Hewa,” alisema Kiran Pereira (THE FOUNDER OF SAND STORIES). Katika maeneo mengi ya dunia mchanga umekuwa hadimu na kusababisha kuibuka kwa vikundi vya watu kama vile smuggling Bands or Sand Mafias. Watu wanaongoza na kumiliki kikundi cha Sand Mafias ndio hao hao wanaomiliki biashara kubwa za nyenzo za ujenzi (Construction Material Businesses) na majengo marefu huko Bombay nchini India. Sand Mafias mikono yao imepenya mpaka kwenye serikali ya nchi hiyo ni kikundi cha watu wenye fedha na network kubwa serikalini. Lakini Jarida la Times of India liliripoti kuwa illegal sand mining ina thamani ya dola 2.3 Bilioni kwa mwaka, kwa eneo la Tamil Nadu peke yake tu.


Mchanga ni kati ya rasilimali ambazo zipo kwa wingi sana Duniani lakini uchimbwa kwa kasi kubwa sana kuliko kiwango chake cha kujitengeneza upya (Natural Renewal Rate). Duniani kote, biashara ya uchimbaji mchanga inayotambulika kisheria ina thamani ya dola 70 Bilioni sawa na GDP (Gross Domestic Product) ya nchi ya kenya.
NOTE: GROSS DOMESTIC PRODUCT – The Total value of goods produced and services provided in a country during one year.

Singapore ni mfano mzuri wa nchi zenye matumizi makubwa ya mchanga, kati ya mwaka 1990 mpaka 2017 idadi ya watu walioongezeka mijini ni mara mbili kutoka 3 milioni mpaka 5.6 milioni. Eneo la miji limekuwa kutokana na kufanyiwa Land Reclamation kutoka 581.5 square km kati ya mwaka 1960 na kufikia 719.7 square km hivi sasa. Reclaiming kilomita moja ya mraba ya ardhi kutoka kwenye bahari inagharimu karibu 37.5 milioni cubic metres za mchanga.

Katika mwaka 2016 Singapore imeagiza 35 milioni metric tonnes za mchanga kutoka Cambodia. Pia katika mwezi Julai 2017, Cambodia wakazuia mauzo yote ya mchanga kwenda katika nchi ya Singapore. Huku Malaysia, Indonesia na Vietnam tayari wameweka vikwazo kwenye biashara ya mchanga kwenda Singapore, kutokana na vikwazo vilivyowekwa vimepelekea kuibuka na kushamiri kwa biashara ya magendo ya uchimbaji na uzaji wa maliasili ya mchanga. 




THE WORLD IS ONLY SLOWLY WAKING UP TO THE FACT THAT ANOTHER FINITE RESOURCE IS SLIPPING THROUGH OUR FINGERS.
#SANDWARS

Comments

Popular posts from this blog

MTO KONGO (CONGO RIVER) NA SIFA ZAKE

CHURA WA KIHANSI NA SAFARI YA MAREKANI

MANGROVE TREES "(MIKOKO)"